Tuesday, December 4, 2007

Falsafa ya Elimu-Tanzania

Salaam.

Ni muda mrefu sasa tangu nilipokuandikia.Kaisari amenishika ndugu yangu nikileta ubishi watoto watalala njaa.Leo nimeona nitumie tena muda huu mdogo wa lunch nikuandikie japo kwa uchache ili tuweze kujadili kwa pamoja kuhusu falsafa yetu ya elimu.


Mwalimu! Fumbua macho.Amka mwalimu!!!Ndio,tunapaswa sasa kufumbua macho na kuona mapungufu yaliyopo katika katika jamii yetu.Tusiwe watu wenye dhamira nyepesi na kuyafumbia macho mapungufu hayo kwa kujifariji kwa dhana dhahania zinazotokana na utekelwazaji wa “Elimu ya kujitegemea”kama falsafa ya elimu ya taifa letu.


Neno Falsafa ndugu zangu lina maana ya Taaluma inayojishughulisha na kutafuta ukweli wa jambo kwa njia ya kutafakari.Lakini Falsafa ya Elimu ni utumizi wa falsafa na mbinu zake katika kufafanua maswala ya Elimu mfano maana ya elimu katika jamii na namna ya kujifunza.Hoja hii ya falsafa ya Elimu ya taifa inakuja katika wakati ambao kwetu wengi hatukukitarajia.Kipindi kigumu na chenye mabadiliko makubwa ya ya kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni duniani kote jambo ambalo limepelekea watu kadhaa kuibua hoja ya kutaka Mjadala wa Kitaifa kuhusu mfumo wa elimu.” ,sera ya Elimu ya taifa na Lugha ya kufundishia na kujifunzia


Mimi nadhani ni vema kabla ya kwenda moja kwa moja kwenye mfumo wa elimu hapa nchini ni vema tukarudi nyuma kidogo katika falsafa yetu ya elimu.Katika kipindi hiki kigumu ni lazima tuamue sasa katika ugumu huo kuona ni aina ya falsafa ya elimu na ndipo twende katika mfumo mzima wa elimu.Tunapaswa kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya ufanisi wa taifa letu.Lazima tuwe na mwanzo.Na mwanzo ni “Tafakuri”.Tafakuri kuhusu aina ya falsafa itakayotuongoza na kutuletea ufanisi katika dunia yetu,Ile “Dunia Bora kwa watu wote” tunayoitarajia.


Falsafa ya Elimu ya taifa tunayoitaka,itakayoendana na aina ya taifa tunalolitaka ni moja ya maswali

korofi” yanayonigonga kichwa kila uchao.Ila kama walimu hatuna namna ya kuyakwepa maswali ya aina hii.Ni lazima kama sehemu muhimu ya jamii tujifunze kuwa na utamaduni wa kujiuliza maswali ya aina hii.Tujiulize tukiwa na dhamira ya kuyapatia ufumbuzi na si vinginevyo.


Matharani,tunapoiangalia falsafa yetu ya elimu kwa sasa”Elimu ya kujitegemea” ni vizuri tukarudi nyuma na kusawiri /kuyaelewa mazingira yaliyopelekea kuibuka kwa kwake ambayo ni kutangazwa kwa Azimio la Arusha.1967,pale tulipoamua kufuata siasa ya “Ujamaa na kujitegemea” ambayo imejengeke katika misingi ya Usawa wa Binadamu na kufutwa kwa unyonyaji.


Ili kufanikisha siasa ya ujamaa na kujitegemea,falsafa ya elimu ya kujitegemea ilitangazwa ili kuwajenga Watanzania katika misingi ya kijamaa.Lengo likiwa ni kumkomboa Mtanzania kutokana na Ukoloni mkongwe,kuwafanya watu wawe huru na kuwa na uwezo wa kujitegemea.


Miongo kadhaa sasa tangu Azimio la Zanzibar lilipopitishwa ili kuthibitishwa Arusha kupewa kisogo ilihali bado tunajidai kutekeleza falsafa ile ile iliyotokana na Azimio la Arusha.Falsafa yetu ya elimu katika Dunia ya leo inakosa mantiki kwa sababu mfumo wetu wa elimu haumtayarishi kijana wa kitanzania kuwa na moyo wa kujitolea na wa kizalendo kama ilivyokuwa imekusudiwa na badala yake umeua moyo wa ushirikiano na kuyashawishi maendeleo binafsi.Hii ni kutokana na ukweli kuwa tunaifuata falsafa ya elimu ya kujitegemea kwa nadharia wakati tukitekeleza kwa vitendo falsafa ya elimu ya “Kidhalimu”


Ujenzi wa mfumo mpya wa elimu kulingana na Mabadiliko ya jamii ya sasa na ijayo ni lazima ujiegemeze katika dhamira moja kuu itakayotokana na kuwa na falsafa maridhawa ya Elimu ya Taifa


Friday, October 19, 2007

Teaching Occupation in Tanzania in relation to Professionalism


Leo tena nimeamua kukuandikia ujumbe mwalimu wa Tanzania.Hata hivyo mjadala huu unaweza pia kujadiliwa nasi wote katika jumuia yetu. Mwalimu, nasikia eti zile kauli "zilizopendwa" za ualimu ni wito zinaendelea kupeperushwa hewani.Uzushi huo na wanaodai hivyo usiwasikilize hao!!!!!! Mwalimu,Mobile phone ndiyo iliyonifanya nipate msukumo wa kukuandikia ujumbe huu.Hapo juu nimekuasa usiwasikilize wanaodai kuwa "ualimu ni wito" kwa sababu zifuatazo.Juzi nilipokuwa narudi nyumbani nikiwa katika usafiri wa jumuia kaka mmoja alikuwa akiongea kwenye simu yake ya kiganjani.Sehemu ya maongezi yake alisema hivi,Nanukuu;
.."Yaani wewe hata ualimu tu umekosa?Kwani
ulipata pointi ngapi? eti!! pointi 30?Acha kuzubaa wewe nenda kasomee ualimu!!..
.."


M
walimu! eti ualimu ni wito! nani kasema?kwangu ualimu ni kazi kama kazi kazi nyingine.Labda sasa naanza kufikiri kauli mbadala kuhusu Ualimu.Inawezekana ualimu ni taaluma ya watu walioshindwa maisha!!!?yaani watu waliokosa mwelekeo wa maisha .Kama hivyo sivyo,ni kitu gani kinapelekea watu kufikia hatua ya kusema ".......hata ualimu tu umekosa......"?

Mwalimu! sitaki kuisadikisha nafssi yangu kuwa wewe ni mchovu na umeingia kwenye taaluma ya Ualimu kwa kuwa hukuwa na uchaguzi mwingine wa kufanya maisha mtaani.Kama hivyo ndivyo kwako,Tafadhali usipoteze muda wako bure,AMKA FUNGASHA UENDE!!!!
Nasema tena na tena wajamane! Ualimu ni taaluma kama taaluma nyingine.Ukijaribu kujimuvuzisha katika Oxford Advanced Learners Dictionary(1998) a profession is defined as a paid occupation,especially one that requires advanced education and training.Na kama ulikuwa haujui,ualimu ni taaluma pia yenye sifa na vigezo karibu vyote vya kazi ya kitaalamu kama Carr & Kemmis(1986) wanavyojaribu kubainisha sifa za kipekee za taaluma.Wanasema;Nanukuu.
"........First of all,a profession consist of members whose methods and procedures of working are based on a body of theoretical knowledge and research. Secondly,a professions have ethical codes which govern their members to ensure that they work with commitment towards the well-being of their clients. Thirdly,in order to make sure that they always work to serve the interest of their clients,professions reserve the right to autonomous judgment free from external non-professional control and constraints..."

Ijapokuwa kuna vigezo vingine vingi vinavyopaswa kuzingatiwa katika kuainisha kazi za kitaaluma,bado nasisitiza kuwa Ualimu ni taaluma kama taaluma nyingine .


Samahani mwalimu nisije nikakuchosha ukashindwa kufanya lesson preparation.Hata hivyo naomba unipe dakika chache ili nimalizie ujumbe wangu.Mwalimu! mimi kwa haraka haraka na kwa akili zangu kidogo nimejifunza kitu fulani ambacho walimu tunapungukiwa nacho.Walimu wa Tanzania hatuna chama cha kitaaluma.(Professional Body).What we have is just a trade union(CWT) which have got nothing to do with professionalization of the teaching profession.
Mwalimu ,katika kufikiri nini cha kufanya ili kuipa hadhi taaaluma ya ualimu hapa nchini tujifunze from other professional bodies like that of engineers,medical doctors or NBAA.Kwa kufanya hivyo labda tutaweza kuwazuia watu wasio na taaluma ya ualimu kuthubutu kufanya maamuzi mazito kuhusu mabadiliko ya mitaala ya elimu nchini kama tulivyopata kushuhudia siku za karibuni.

Mwalimu,am very sorry as I am getting confused as I don't know what am I writing.But what I know for sure is that I am writing to mwalimu wa Tanzania.As long as you have the lesson plan,lesson notes and the teaching aids,Please get ready for lesson presentation and lets meet again next time on the discussion about "CWT na Mustakabali wa Elimu na Ualimu Tanzani"

Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania.

Mwenzenu


Wednesday, October 3, 2007

Kimepotelea Wapi kizazi hiki?

Poleni kwa mihangaiko ya hapa na pale.Nimeona si vibaya nikashiriki pamoja nanyi katika kujiuliza maswali ambayo japo sio mara yangu ya kwanza kujiuliza but yaliibuka kwa kasi jana nilipoamua kuingia mtaani pasipo dhamira yoyote baada ya kupata taarifa ya kuahirishwa kwa kikao cha kamati ndogo ya "Infomal network of young Tanzanian Intellectuals (wanazuoni) pale Mzalendo Pub-Kijitonyama.

Kimepotelea wapi kizazi hiki? ni swali nililobaki kujiuliza hata sasa kutokana na yaliyojili katika mazungumzo na watu mbalimbali katika matembezi yangu.

1. Kimepotelea wapi kizazi hiki?

* Kizazi cha vijana wa kitanzania waliokuwa tayari kupingana na itikeli za maisha zilizowalazimisha kuyakubali yale wasiyoyaafiki kuwa ndio msingi wa ujenzi wa jamii wanayoitaka?

* Kimepotelea wapi kizazi cha vijana wazalendo waliokuwa tayari kuifia nchi yao kwa kuipigania kwa kwa lolote waliloamini ni kinyume na matarajio ya jamii yao?

* Wapo wapi wanawake ambao walikuwa tayari kusema hapana kwa mali na ndio kwa mapenzi ya dhati katika hali iwayo yote ile waliyonayo hao wawapendao?

* Kimepotelea wapi kizazi cha wanawake wenye huruma ambao hawakuwa tayari kuharibu mimba ya watoto waliowabeba?

* Kizazi cha wanawake waliokuwa tayari kubeba mimba miezi tisa na kulea watoto wao?

* Wanawake waliokuwa tayari kulea watoto wa wengine?

* Kizazi cha wanawake waliokuwa tayari kuanza maisha ya pamoja na wenzi wao/waume zao/wao wakiwa hawajui waanze vipi?wakiwa hawana hiki wa kile,waliokuwa tayari kuwasubiri wenzi wao kuwa muda wowote wawapo mbali na upeo wa macho yao?

* Kimepotelea wapi kizazi cha kile ambacho wazazi na walezi waliokuwa tayari kuwaonya watoto wa wengine waliowaona wakipotoka popote walipowaona?

* Kikowapi kizazi cha watoto wale waliokuwa taayari kuacha michezo yao na kuwasaidia wazee wasiojiweza na wote waliowazidi umri mizigo yao hadi wakotaka kufika na kurudi kuendelea na michezo yao?

2. Wazazi kwanini mmeacha kuzaa kizazi hicho?au
mmekwenda likizo ya uzazi
hadi hapo mtakapobaini kiu ya uhitaji wa Dunia kuwa
na watu wa aina hiyo?

3. Je,ni wakati gani huo mnao usubiri kama sio sasa?

4. Wakunga kwanini mmeacha kuzalisha watu aina hiyo
ilihali Tanzania,Africa na Dunia inawahitaji?


* Je,hali hii itaachwa hadi lini?
* Intellectuals wanafanya nini kuinusuru jamii kutoka katika ghalika(Angamizo kuu)

Aaah!Dhambi hii tutaungama wapi?

Mwenzenu,
Malata

World Teachers Day:How do you find it?


Hallow Mwalimu,
Pole na majukumu yako ya kila siku.Kwa muda mrefu nimekuwa kimya pasipo kukuandikia kutokana na ndoa yangu na Kaisari kutoashiria kuwa na mashaka jambo linalonifanya nijibidiishe sana katika kazi ili niweze kumshawishi asinipe talaka.

Leo nimeamua kutumia muda huu mdogo wa chai kukuandikia japo kidogo.Siku ya mwalimu Duniani ndiyo iliyonipa morali wa kukuandikia Mwalimu.

Tarehe 5 Oktoba ya kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya Mwalimu.Siku hii kwa hapa kwetu Tanzania huratibiwa na kudhibitiwa na Chama cha walimu Tanzania(CWT) .Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu sana maadhimisho hayo kila mwaka tangu nilipotambua kuwa kuna kitu kama siku ya mwalimu.Hivi mwalimu unatambua kweli kiini cha siku hii ya mwalimu na madhumuni yake?

Katika maadhimisho yote niliyopata kuhudhuria katika mikoa ya kanda ya mashariki kikubwa kinachofanyika katika maadhimisho hayo huwa ni maandamano, mashindano ya kufukuza kuku,kutembea ukiwa ndani ya gunia,mashindano ya kula,ngoma za kuhamasishana ,kwaya,riadha na mashindano mengine yanayoonekana kufaa kwa wahusika.Mwisho wa yote huwa ni-kujimuvuzisha kwenda mahali fulani kwa wahusika fulani kwa ajili ya "kukata mti na kupanda mti" vijana wa kijiweni wanaita "Kujiachia"

Mwalimu,hapo juu nimekuuliza hivi kweli tunajua kiini cha kuanzishwa kwa siku hiyo na madhumuni yake?Mimi sijui ila bado najaribu kutafuta ukweli katika hilo.Inawezekana waratibu wake hapa nchini(CWT) wanajua.Katika ujumbe wangu huu kwako leo sitaki kabisa kugusia kuhusu CWT na Mustakabali wa taaluma ya Ualimu na Elimu Tanzania kwani ni mada nitakayoizungumzia siku nyingine kipekee.Ila ombi langu kwako ni mabadiliko ya "kimtazamo kuhusu siku ya mwalimu."

Mwalimu! nazungumzia kubadili mtazamo kutoka katika kuadhimisha kwa kufanya mambo tuliyoyazoea na kuangalia namna tunavyoweza kufanya-Professionalization of Teaching profession kwa kutumia siku hii ya mwalimu.Hili linawezekana ikiwa tu walimu wataandaliwa na kupewa nafasi ya kuandika papers na kuziwasilisha katika maadhimisho hayo katika ngazi zote.Yaani kuanzia katika vituo vyao vya kazi hadi kitaifa.Teana ikiwezekana hapa kwetu tuwe na wiki ya mwalimu badala ya siku ya mwalimu.Kwa mwaka huu unaweza kuwa umechelewa kwa kuwa zimebaki siku tatu tu kama sijakosea.Lakini ni matumaini yangu kuwa hii ni nafasi yako kujadili na mwalimu mwenzako na kufikisha ujumbe huu kwa walimu wengine na kuona ni kwa namna gani tunaweza kuifanya siku hii ya mwalimu kuwa ni yenye manufaa zaidi kwa taaluma ya Ualimu na maendeleo ya Elimu nchini.

Mwenzenu,

____________ _________ _________ _________ _________ _________ _
Without "Ethical Culture" there is No Salvation for Humanity
____________ _________ _________ _________ _______

Tuesday, September 18, 2007

Social Responsibility,Parliament and the Role of Intellectuals

The recent events have created the need for a re-examination of our Society in general and the parliament in particular.While the "Udanganyifu" reporting scandals such as the one which involved Hon.Adam Malima Vs Mengi and Zitto Zuberi Kabwe Vs Hon.Nazir Karamagi and "Ufisadi" katika BoT have been dominating headlines recently,the crisis of confidence resulting from the ongoing scandals is really a symptom of deeper issues that need to be addressed.

What is the deepest issue affecting the survival of the parliamentary system?Clearly, the public perception that criminals,whether of the corruption or else,will not be adequately punished by neither parliament nor justice system.This perception,and the parliamentary decisions that feed it,brings the credibility of the social order into question.

What is the problem with the parliamentary system of Tanzania?This crisis has resulted because the parliamental system is overly focused on traditions such as Itikadi za kichama and what is known as "Umimi" if Not "Ubinafsi".

Samahani I am truly one of the "Swa-english" so be patient when am trying to make clarifications on some concepts.Now, with respect to the subject above,lets examine a bit the recently events.

Matukio ya hivi karibuni yaliyoibuliwa bungeni,particulary hili la kusainiwa kwa mikataba ya madini nje ya nchi na reaction ya baadhi ya wabunge,spika, naibu spika na kukomelewa msumari na karani wa Bunge against mtoa hoja ya msingi(Mh.Zitto) na mwitikio wa jamii kuhusu uamuzi uliochukuliwa na Bunge ni ishara mbaya kwa mwelekeo wa nchi yetu.Imefika wakati sasa,eti Bunge linathubutu kuzuia wawakilishi wa wananchi(Wabunge) na wananchi wenyenye nje ya bunge kujadili mambo yanayowahusu kwa kisingizio cha kuingilia shughuli za Bunge ambalo siku za hivi karibuni limekuwa mithili ya "Kijiwe cha wahuni" kiasi cha kuamua kusigina kanuni zilizowekwa kusimamia shughuli za chombo hicho.
{Rejea kanuni za uendeshaji shughuli za Bunge;kanuni ya 28(1);kanuni ya 44(1);kanuni ya 68(1) na kanuni ya 103(2) against uamuzi uliochukuliwa na chombo hicho dhidi ya Mh.Zitto.}

Wote tunaojua kazi na majukumu ya Bunge tunaelewa wazi kuwa "Kuwanyamazisha wananchi" sio kazi ya Bunge.Ikiwa basi tunaamini kuwa "Msomi" ni yule aliyeenda shule(Formal schooling),basi Bunge letu limesheheni wasomi waliotukuka katika fani mbalimbali.The challenging question remains;What is our role and relevance as Tanzania Intellectuals?

Joseph Mihangwa,mmoja wa waandishi makini wa makala nchini aliwahi kuandika kumwelezea "msomi" kama ifuatavyo;-
"Msomi yeyote anawajibu wa kuelewa na kujihusisha kikamilifu na mambo yote yanayotokea katika jamii yake,na hupimwa uwezo wake kwa jinsi anavyojishirikisha na tabaka la watawala kama yeye si mtawala katika kuleta hali boramkwa jamii yake.

Msomi hapaswi kusubiri kuambiwa afanye nini hali tata inapotokea katika jamii yake.Yeye ni mwepesi wa kutenda na kuleta mabadiliko yanayotakiwa. Ni wajibu wake kuongoza na kushiriki kikamilifu katika kuleta mabadiliko hayo.Kutofanya hivyo ni uasi kwa jamii unaovuka kiwango cha Uhaini na hivyo hawezi kukwepa kujibu tuhuma za kuiasi jamii yake"
{Wasomi kizimbani,Rai No...,Feb. 27,2003}

Ninapojaribu kutafuta uhusiano wa aina ya watu tulionao ndani na nje ya Bunge,na yale yanayotokea hapa nchini,I come up with the conclusion that "What is missing is an emphasis on social responsibility"

What is meant by social responsibility?Social responsibility involves taking into account the needs of society;the damage to society of the crime;and the impact of any decision on the fabric of that society.The health of the Society is paramount.Note, that does not mean that society can trample on individual rights...that would only negate any social purpose.Rather, it means that individual rights can exist up to the point where society becomes threatened.That does not mean social change cannot occur...since social change is healthy and reflects a vibrancy in that society.Again, it means that society cannot be taken advantage of,in particular for ulterior purposes.

If social responsibility does not become an important consideration in the parliamentary system,them the bleeding of public confidence will continue---and that will serve neither the parliamentary system nor society.Kindly I keep the ball rolling.

Collegially

Pro.Chachage:Msomi wa Jamii ataekumbukwa Daima


Ni mwaka wa tatu  sasa tangu mpendwa wetu Prof. Seithy Chachage alipoiaga dunia. Leo ni siku ya kihistoria kwetu. Ni siku ya kihistoria kwa kuwa tunaadhimisha kumbukumbu ya kifo cha mpendwa wetu, mzazi wetu, mlezi wetu na rafiki yetu. Siku ya leo ni siku inayotuongoza kuyatafakari mambo machache katika maisha yetu yanayoguswa na maisha ya Profesa Chachage (Mungu amlaze mahali pema). Ni siku ya kugeuka na kutazama haiba ya jamii yetu tukizingatia yanayojitokeza katika utashi wa waliotutangulia. Kumbukumbu hii inafanya historia kwetu isiwe mambo ya kale ila mambo yanayotuhusu sasa na kwa matarajio mema ya siku zijazo.

Kwa hiyo basi, historia kwetu iwe ni sasa ikivuviwa na zamani; iwe ni matendo ya sasa yakitiwa nguvu na yale ya waliotutangulia Tunapofanya tafakuri ya maisha ya marehemu Profesa Chachage, ni vema tukaungana na wanafalsafa waliojaribu kuiona historia kama tendo la mtu anayekimbia, akienda mbele anakotaka bila kupafahamu, ila akitazama nyuma kwa tahadhari ya yaliyoishakumgusa.

Kumbukumbu ya leo inatusukuma kuifikia hali ya ukingoni ambayo wanatheolojia wanaiita “ apocalyptic moment”. Hali inayodai ufunuo mpya. Hali tata inayodhihirisha fumbo la maisha yetu . Fumbo hili ni kwamba, kuna pengo kubwa kati ya ukweli wa maisha yetu na jitihada za mantiki tunayotumia ili kuona ukweli huo . Ndio maana tunasimama na kutafakari ;tunatazama maisha ya waliotutangulia ili kupata nguvu za utashi wa sasa unaokidhi haja za kisasa. Tunatafakari maisha ya Profesa Chachage ili tuweze kuyaona maisha yetu vizuri zaidi .Ni kipindi cha kutafakari!

Ujasiri wetu wa kutafakari maisha ya Profesa Chachage huenda ukafananishwa na ule wa Susi na Chuma waliotafakari maisha ya Dr. David Livingstone na kuubeba mwili wake toka Ujiji – Kigoma hadi Bagamoyo akazikwe makwao. Sisi tunatafakari maisha ya mtu aliyeishi pamoja nasi , aliyefanya kazi pamoja nasi. Tunamkumbuka Profesa Chachage kwa mshikamano aliokuwa nao kwetu hadi kufikia mauti yake.

Pamoja na ukweli kuwa ni mwaka mmoja tu tangu alipotutoka,mengi yanayotuzunguka huibua kumbukumbu kumhusu Profesa Chachage. Wengine tumeishi naye ; wengine tumefanya kazi pamoja nae na wengine tumemsikia tu na kuona kazi zake. Hayo yote hudhihirisha azma aliyokuwa nayo katika maisha yake aliyoishi kama “Msomi wa Jamii (Public Intellectual)”

Ninaporejea hotuba kali yenye simanzi ya William Shakespare katika tamthilia ya Julius Kaisari inaonyesha ujasiri wa Marko Antoni katika kumzika Kaisari “…….. maovu watendayo watu hudumishwa baada ya uhai wao , ila mema huzikwa pamoja na mifupa yao…………” Na iwe hivyo kwa Kaisari!”Marko Antoni alisema hayo kwa kuwashutumu mahasimu na Waroma kwa kusahau mema mengi ambayo Kaisari aliwatendea. Nasi leo tunajaribu kuyataja walau machache katika mema mengi ya Profesa Chachage.

Kwa hakika yapo mambo mengi sana mema aliyoyafanya Profesa Chachage katika siku za uhai wake. Profesa Chachage katika uhai wake alijitahidi sana kuitazama haiba ya jamii yetu kwa kuzingatia mambo yanayojitokeza katika utashi wa matendo yetu ili kuleta ufunuo mpya na matarajio mema ya jamii yetu kwa siku za usoni.

Profesa Chachage aliitambua fika “ajali” yetu; ambayo ni kuishi katika bara lililojaa mazonge na madhila, na mzigo wa umaskini. Siku zote alikuwa ni mfuasi mzuri wa dini ya “Ubinadamu” akijitahidi kuikarabati jamii na kupanda mbegu ya ujasiri ili tuweze kuikana mifumo dhalimu inayowalaza watu njaa. Aliamini kuwa tunahitaji uhuru wa fikra na juhudi zetu wenyewe katika kujiletea maendeleo .

Siku zote alikinzana na wasomi wetu ambao wengi wao wamenaswa katika mikoba ya uchawi wa Giningi na kusahau kabisa uganga (Udaktari) ambao wameusomea na kufuzu kwa viwango vilivyotukuka. Alipinga wazi wazi matendo yaliyopanua mpasuko katika jamii baina ya watawala wakwasi wa kupindukia na wananchi maskini hohehahe waishio katikati ya utajiri wa asili.

Kutokana na hulka aliyokuwa nayo ,sio tu aliwaogofya watawala “waliokeneguka” bali pia asasi za kimataifa kila alipokuwa akitoa mwito wa kujali masuala yahusuyo ujenzi wa jamii bora yenye kuzingatia haki , usawa wa binadamu, uhuru , ubinadamu na ukomavu wa kiuchumi. Pamoja na ukweli kuwa juhudi za kujikomboa katika nyanja zote za kujenga Dunia mpya iliyo bora. Mapambano ya kuleta Dunia mbadala ambayo haina ubaguzi, ukandamizwaji, unyonyaji wala ufisadi ina historia ndefu , tangu enzi za mababu zetu. Inasikitisha kuona kuwa kila kukicha wajanja wanakuja na mifumo mipya ya maisha inayotutaka turudi nyuma katika mapambano haya ya kihistoria.

Profesa Chachage hakuna alichopoteza duniani. Alifanya mambo mengi makubwa kwa ajili ya nchi yetu na kuweka “muhuri” wake katika mioyo ya Watanzania. Kama ilivyo kwa shujaa wa “Mapinduzi” Che Guevara , Profesa Chachage tutaendelea kumkumbuka kwa ushujaa wake. Ushujaa wa kuchukua uamuzi mzito kwa ajili ya watu na si wakubwa fulani. Maombolezo ya kifo chake na umati wa watu waliohudhuria mazishi yake ni ushuhuda wa haya yanayosemwa juu ya Profesa Chachage.

Kwa haraka haraka, anayesikiliza tafakuri hii ya maisha ya Profesa Chachage anaweza kusema kuwa inamhusu mtu mmoja mdogo na mahala fulani padogo (Mtwango au Changanyikeni)! Ikumbukwe kuwa wengi tumepita mikononi mwake na kusambaa katika jamii pana. Kwa njia hii maisha ya mtu mmoja yanaweza kuwagusa wengi hata wale ambao hawakukutana nae. Kutafakari kwetu kutukumbushe mbegu ya haradali.
Ni mbegu ndogo sana, ila hupandwa na kuchipua . Inastawi na kuwa mti mkubwa ambao ndege hutua na kuimba juu yake. Mbegu moja huzaa maelfu na kutokana nayo hupatikana msitu mzito.

Kwa hakika leo hatuombolezi. Hatuna majonzi katika kumkumbuka Profesa Chachage . Jambo lililo muhimu kwetu sasa ni kwamba, katika kumkumbuka tunaweza kuchipuka upya kama mbegu ya haradali. Tujifunze kuwa tayari kusimama , kuhoji na kukataa mambo yote yanayotulazimisha kuyakubali yale tusiyoyaafiki .Mambo yanayopingana na itikeli za maisha yetu. Kumbukumbu ya Profesa Chachage inatukumbusha kuepuka kujiuliza, “Nitapata nini nikitenda mema? Hiki ni kipindi kinachohitaji ufunuo mpya!

“Mungu amlaze mahali pema peponi Profesa Chachage”

Adios Amigo

Profesa Seithy Loth Chachage “Mwamwani”