Sunday, December 21, 2008

Food Quality and Safety Evaluation Workshop in Pictures

The permanent secretary,Ministry of Education
and Vocational Training Hon Hamis Dihenga
Giving the opening speech to the participants.

Some of the workshop participants atentively
listening to the guest of Honour .

Ms. Georgina Cattaneo,UNIDO Representative
addressing to the participants during the opening ceremony.

The guest of Honour.The Permanent Secretary MoEVT Hon.Hamis Dihenga in a group photo with the workshop participants 5th from light.To his light hand side the Ag. Directo secondary education,Ag director TBS ,Principal Vikindu ttc Mrs T.W. Rwechungura and the Unido observaer.

Mama Mbonya,the workshop facilitator from
Tanzania Institute of Education facilitating group
discussion during the session.

The workshop participants actively participating
in the discussion of the issues of food quality and safety
as they have raised during evaluation.

Ag.Director of secondary education giving a certificate
to theHeadmistress of Kilakala secondary school.
Kilakala sec. was a general winer of the
Food quality and safety competation.
UNIDO oficials,TBS as well as MoEVT oficials
and the Winners of the food quality and safety
competations in a group photo with the
Ag.Director of secondary education department
who was a guest of honour during the closing of the workshop.
It was all about Food quality and Safety
[Chakula bora Chakula salama]

Tuesday, September 30, 2008

CWT kwa maslahi ya nani?Walimu,Serikali au Viongozi?

Mwalimu House ni moja ya majengo mazuri yanayoupamba mji wetu wa Dar si salama.Picha hii inayoonekana hapo ilichukuliwa wakati ujenzi wa jengo ukiendelea.Mwalimu House ni jengo linalomilikiwa na chama cha Walimu Tanzania [CWT]. Ni moja ya miradi mizuri iliyobuniwa na chama katika kuendeleza na kutunisha mfuko wa chama.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na mijadala mikali katika mitandao ya kompyuta kuhusu mapato na matumizi ya fedha za chama.Kwa hakika sijui kusudio hasa la madai hayo ingawa wengi wa wachambuzi wa mambo wanayaelezea kama sehemu ya serikali kupitia kwa watu wake kujibu mapigo kwa viongozi wa chama ambao mara nyingi wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania maslahi ya walimu nchini.Jambo hili linakuwa ni rahisi kuingia akilini mwa watu kutokana na ukweli kuwa madai ya wanachama hao wachache yamekuja siku chache tu baada ya chama kusimama kidete kuishinikiza serikali kulipa madeni yote ya walimu kwa muda muafaka japo bado hilo halijafanikiwa ipasavyo.

Aidha,mjadala mwingine wenye madai mazito kuhusu makato ya ada za uanachama wa CWT ambayo inakatwa kwa asilimia ya mshahara wa kila mwanachama na serikali kutuhumiwa kuhusika katika kushinikiza kila mwalimu awe mwanachama wa CWT na michango yao kukatwa moja kwa moja na Hazina kinyume na taratibu za trade union zingine duniani ni kizungumkuti kingine kwa CWT na serikali kwa ujumla.

Nisingependa kuzungumzia sana kuhusu jengo la mwalimu house wala aina nyingine yoyote ya kitega uchumi cha CWT. Ila nalazimika kuchangia kuhusu makato ya ada ya uanachama na aina za wanachama wa CWT.Kwa maoni yangu nadhani huu ni wakati muafaka kwa serikali na CWT wenyewe kuangalia upya kiwango cha ada ya uanachama ambayo kila mwanachama atapaswa kuchangia tofauti na ilivyo sasa ambapo kiwango cha ada hutofautiana kulingana na kiwango cha mshahara wa mtu.Trade union zote ninazozifahamu zinatoza Ada ya uanachama kiwango kilicho sawa kwa wanachama wake wote.

Aidha kuhusu uanachama wa CWT katiba ya chama ipo wazi .Imejaribu pamoja na mapungufu yaliyopo kufafanua nani ni mwanachama na aina za uanachama.Kutokana na hali hiyo ni vema kwa chama kuitetea na kufuata katiba yake kwa kuwatoza ada ya uanacha wale tu wanaoitwa wanachama hai na sio kumkata kila mwalimu ada ya uanachama kwa kisingizio cha taaluma yake ya Ualimu.Jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa wengi wa wanaokatwa ada hiyo ni walimu wale tu walio watumishi wa serikali kwa kuwa ni rahisi sana kujimegea kamkate kao kutoka hazina jambo linalotufanya wengi tujiulize chama hiki ni kwa manufaa ya nani?Je, hizi kelele zinazopigwa na viongozi wake zinamaanisha nini ikiwa chama na serikali lao moja?Kwa hakika mimi sijui.

CWT na serikali kwa ujumla nadhani huu ni wakati muafaka wa kujipeleleza na kuangalia nini cha kufanya kabla jeshi hili kubwa zaidi la watumishi wa umma nchini halijainuka na kuleta dhahama kubwa.Ndio wataamuka tu muda sio mrefu.Wengi wao hasa wa kuanzia miaka ya mwishoni mwa 1990s` hawajawahi kuingia mkataba na CWT kuwa wanachama.Hawana membership number wala kadi.Je,wakidai warejeshewe makato yao tangu walipoanza kazi na kukatwa ada isivyo halali watakuwa wamekosea?Hili ni bomu linalotakiwa kuteguliwa haraka iwezekanavyo. Na kwa nini tusubiri hali hiyo itokee.

Kazi ya mja kunena nami nimenena.

Tuesday, August 5, 2008

Tutors & Secondary school teachers attends the food quality & Safety workshop




Early last month,Tanzania Bureau of standards [TBS] in collaboration with United Nations Industrial Development Organization[UNIDO],Tanzania Institute of Education [TET] and Ministry of Education and Vocational Training [MoEVT] conducted the training workshop to selected Home Economics and Biology secondary school teachers and College tutors from Eastern zone on Food quality and Safety at VETA center,Morogoro as a part of the National food safety campaign.


The workshop intended to orient Home economics and Biology secondary school teachers and tutors on how to integrate the knowledge of food quality and safety in teaching their respective subjects.


Ms Giorgina Cattaneo,the UNIDO representative on her remarks said that the aim of the workshop was to equip teachers and tutors with relevant knowledge on food quality and safety issues and enable them to deliver to their students the basic rules and best practices to apply in ensuring food quality and safety throughout the food chain and food ultimately protection to their family`s health from food born diseases,contribute to food security as well as to raise awareness on fair practices in food trade.


In that occasion, Mr. Ekerege,f. From Ministry of Education and Vocational Training who was the workshop coordinator said that the workshop was organized in the context of the awareness campaign targeting secondary school students as well as student teachers due to the fact that secondary school students and student teachers represents both future stakeholders, to include not only food producers,processors and marketers but also consumers as well in the country. It is therefor vital to ensure that information about food safety and quality is provided to them.


Official opening of the workshop was done by Mr.Musaroche,L. The acting chief Education Officer MoEVT. In his speech,Mr. Musaroche said that the government expectations to the workshop is the fulfillment of the project objectives which are mainly to reduce as far as possible,cases of food borne illness or disasters in the country resulting from consumption of unsafe food which lead to reduces productivity nationwide.


The workshop was very successful and the participants awarded certificates of attendance awaiting for implementation and evaluation of the project.


Monday, July 28, 2008

Chakula Bora chakula Salama katika picha


Workshop participants in a group photo with the Guest of Honour Mr.Musaroche,the acting chief Education Officer,MoEVT.



One of the Participant from Ifakara secondary school leading the discussion on how to intergrate the chakula bora chakula samala contents in teaching of Biology lesson


The Home economics teacher showing how to intergrate the chakula bora chakula salama content in teach their lesson



Mr.Massaga of TBS and Mama Mbonya of TIE facilitating the discussion

The Guest of Honour awarding a certificate of attendence to one of the workshop paticipant during closing cerimony.



The workshop participants in a group photo with the guest of Honour soon after clossing the workshop

Thursday, July 17, 2008

Washiriki wa kozi ya ICDL katika picha.

Aliyekuwa mwenyekiti wa sekretarieti ya wakufunzi waliohudhuria kozi ya ICDL kituo cha Mpwapwa Ndg.Kidumu J.O akitoa muhtasari wa mafunzo hayo kabla ya kumkaribisha mkuu wa chuo cha Ualimu Mpwapwa Ndg Jumbani kuhitimisha mafunzo.
Hapa mkuu wa chuo cha Ualimu Mpwapwa ndg Jumbani akitoa mawaidha siku ya kuhitimisha mafunzo ya ICDL kwa wakufunzi waliokuwa kituo cha mpwapwa

Washiriki wa kozi hiyo wakifanya maandalizi ya mwisho tayari kwa mtihani.

Somo hapa limekolea


Baadhi ya wakufunzi waliokuwa katika kituo cha Mpwapwa Tc wakiwa katika picha ya pamoja tayari kwa safari UDSM kwa ajili ya mitihani ya ICDL

Friday, July 4, 2008

“Ukinyonga” wa Serikali kuhusu Machapisho ya Kufundishia na kujifunzia.

Leo nimeona niandike kuhusu machapisho yanayotumika katika kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi,sekondari na vyuo vya ualimu hapa nchini.Msingi na chimbuko la makala haya ni “Ukinyonga” wa serikali kuhusu uchapishaji wa machapisho hayo..

Mwanzoni mwa miaka ya tisini tulishuhudia kuzikwa kwa azimio la Arusha na Kuzaliwa kwa Azimio la Zanzibari ambalo liliimarisha[sio kuanzisha] na kuendeleza “wimbo” mashuhuri wa Uhuru wa biashara---soko huria---.Hivyo kumaliza ukiritimba wa baadhi ya taasisi hasa za serikali katika soko jambo lililotuingiza katika zama hizi za “ulaji na uteja”.Hii inatokana na ukweli kuwa serikali kwa dhati iliamua sio tu kutekeleza kwa vitendo sera ya soko “holela” bali pia kujiondoa katika ushindani wa soko [kwa kubinafsisha mashirika ya umma] na kuiachia sekta binafsi.

Kuanzia mwaka 1995 hadi 2000+ tumeshuhudia mabadiliko makubwa katika sekta ya Elimu yaliyotokana na sera ya elimu na mafunzo ya 1995.Matokeo ya sera hiyo yalipelekea kuundwa kwa kamati maalumu ya kutathmini machapisho ya kielimu[EMAC] chini ya Wizara ya elimu katika idara ya Sera na Mipango(Rejea waraka wa elimu Na.2 wa 1998)

Kwa mujibu wa waraka huo machapisho yote yanayotumika kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia katika shule za msingi,sekondari na vyuo vya ualimu Tanzania bara hayana budi yaidhinishwe na wizara ya Elimu kupitia EMAC [Ingawa yale yote yaliyoandaliwa na TET hayana ithibati].Baada ya upembuzi yakinifu na utafiti wa kina kufanyika,serikali kupitia waraka wa Elimu namba 7 wa 2005 iliamua kuipa nguvu zaidi EMAC ili kudhibiti ubora wa machapisho ya kielimu hapa nchini.

Yabidi tufahamu kinaga ubaga ninamaanisha nini hasa ninapozungumzia ukinyonga wa serikali kuhusu machapisho ya kielimu.Kabla ya mabadiliko ya “hali ya Hewa” katika sekta ya elimu nchini,machapisho yote ya kielimu yalitolewa na kusambazwa na Taasisi ya elimu ya Taifa [TET] ambayo imepewa mamlaka kisheria ya kuandaa,kukuza,kusambaza,kusimamia na kutathmini mitaala ya shule za msingi,sekondari na vyuo vya Ualimu hapa nchini. [Rejea Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 sura ya 6 uk.51 Ibara ya 6.2.1]

TET ni taasisi ya serikali iliyochini ya Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi (MoEVT). Taasisi hii iliundwa kwa sheria Na. 13 ya 1963 wakati huo ikijulikana kama Taasisi ya Elimu(Institute of Education) chini ya chuo kikuu kishiriki cha Dar es salaam.Pamoja na mabadiliko mbalimbali kufanyika,mfano ya kuwa chini ya chuo kikuu cha Dar es salaam na kubadili jina kutoka iliyokuwa taasisi ya elimu na kwenda Taasisi ya ukuzaji mitaala [Institute of Curriculum Development] na sasa Taasisi ya Elimu ya Taifa [Tanzania Institute of Education] malengo ya uanzishwaji wa taasisi hii,kazi ,dhima na dira yake hazijabadilika.

Serikali katika moja ya harakati zake za kujiondoa katika ushindani wa soko kupitia wizara ya Elimu na utamaduni (Sasa Elimu na mafunzo ya ufundi) chini ya Mpango kabambe wa maendeleo ya sekta ya Elimu,mwaka 2004 iliamua kuingia makubaliano na sekta binafsi ili kuziachia kazi za kuchapisha kuuza na kusambaza machapisho yake yote ya kielimu yaliyokuwa yakitumika katika shule na vyuo vya ualimu nchini.Aidha,katika kutimiza azma hiyo serikali ilitangaza zabuni na kuingia mikataba na makampuni binafsi ya uchapishaji kwa lengo la kuyauzia hifadhi yake ya vitabu vya kiada.

Pamoja na ukweli kuwa serikali ilijitoa katika uchapishaji na usambazaji wa vitabu vya kiada,ziada na rejea,wapo watu wanaoendelea kuulilia “Ukale” na kuitaka serikali irudi katika biashara [Kwa faida ya nani?!].Katika kutaka kutimiza ndoto zao hizo wanatumia nguvu nyingi na fedha za walala hoi kufanikisha azma hiyo.

Kwa harara ya Faru kama sio Mbogo,serikali imeyapokea mapendekezo yao na katika kujaribu ku-justify papara iliyonayo Taasisi ya Elimu ya Taifa [TIE] kupitia kwa kampuni ya ENV consult (T) ltd katika barua yake ya June 20,2008 yenye kumb.Na.TIE/CR/644/08/I/12 imesambaza waswali hojaji [Dodoso] kwa wazazi,wanafunzi,walimu na asasi mbalimbali kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali zitakazosaidia kile wanachodai kuboresha utendaji wa Taasisi hiyo [Katika uandaaji wa vitabu?!!] ili kukidhi kusudio la uanzishwaji wake.

Nashawishika kusema kuwa utafiti huo ni sehemu ya namna ya ku-justify papara ya serikali kutokana na hofu yangu kuhusu uthabiti wake.Hii inatokana na ukweli kuwa madodoso hayo ambayo kwa sehemu kubwa [Taz swali la 8-13 ]yanalenga kubaini ubora wa vitabu yanapita katika mikono ya watu wengi (Wazazi,wanafunzi na hata baadhi ya walimu) ambao misingi na vigezo vya uchambuzi wa vifaa vya mtaala hawavijui.

Katika kuutafakari ukinyonga wa serikali kuhusu shughuli ya uchapishaji na usambazaji wa machapisho ya kielimu ni vema tukakumbuka kuwa Uamuzi wa kujiondoa ulitokana na pamoja na mambo mengine matakwa ya sera ambayo iliandaliwa baada ya tafiti mbalimbali na za kina kufanyika.

Ninapata Mkanganyiko pale ninapojaribu kutafakari kazi na wajibu hasa wa Taasisi ya Elimu na Uanzishwaji wa EMAC.Aidha,sioni mantiki ya chombo hicho “kuegeshwa” katika idara ya Sera mipango wizara ya elimu badala ya kuwa kitengo katika Taasisi yenye mamlaka na mitaal.In maanisha nini kuueleza umma kuwa TIE pamoja na mambo mengine ina wajibu wa kusimamia na kutathmini mitaala wakati kazi ya kutathmini na kuidhinisha machapisho ya kielimu inaachiwa chombo kingine?! Au ni aina nyingine ya Ufisadi?Kwa nini TIE ing`ang`anie kutunga vitabu na kuacha jukumu lake la msingi kabisa?

Siku za hivi karibuni kumekuwa na malalamiko kuwa machapisho mengi yaliyoko sokoni hayana ubora unaotakiwa!Jambo la kusikitisha ni kuwa malalamiko hayo yanatolewa na watu waliopewa dhamana ya kuangalia ubora huo.Kihalisia wanaithibitishia jamii kuwa wameshindwa kuwajibika.Hivi inakuwaje bidhaa mbovu zikaidhinishwa na kupewa ithibati wakati chombo cha kusimamia kipo na miongozo ua uthamini ipo na watu wanalipwa mishahara?achilia mbali posho ya kazi hizo?
Hainiingi akilini!!! Ahhh!!!!!!!!


Mungu ibariki Tanzania.

Saturday, June 14, 2008

Asilimia 13 hawajui kusoma, kuandika’

IMEELEZWA kuwa zaidi ya watu milioni 5, sawa na asilimia 13 ya Watanzania takriban milioni 36, hawajui kusoma na kuandika.

Hayo yalisemwa hivi karibuni mjini hapa na Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Watu Wazima na Mratibu wa Elimu kwa wote kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Salum Manjagila, alipokuwa akizungumza katika mkutano wa uhamasishaji wa progaramu ya Ndiyo Ninaweza, katika Manispaa ya Dodoma.

Alisema kuwa idadi ya watu wasiojua kusoma na kuandika nchini imekuwa ikiongezeka kwa asilimia mbili kila mwaka, hali itakayosababisha idadi ya wasiojua kusoma na kuandika kukua iwapo hatua za kukabili hali hiyo hazitachukuliwa.

Alisema hiyo inaonyesha kuwa watu hawajahamasishwa kiasi cha kutosha kuhusu kujifunza kusoma na kuandika, kama njia ya msingi ya kufuta ujinga.

Manjagila alisema mpango huo unafanyiwa majaribio katika mikoa minne ya Mwanza, Ruvuma, Dar es Salaam na Dodoma.

Alisema lengo la mpango huo ni kuhakikisha kuwa watu wasiojua kusoma na kuandika nchini wanatambuliwa na kupatiwa fursa hiyo, na pia kuangalia maeneo ya kuboresha na kuongeza ubora wa elimu ya watu wazima.

Manjagila alisema mpango huo unagharamiwa na serikali, ambako jumla ya sh milioni 200 zimetengwa kwa ajili ya mafunzo na kiasi cha sh milioni 30 zimetengwa kwa ajili ya kukarabati baadhi ya vituo vya elimu ya watu wazima.

Alisema kuna watu wazima wasiojua kusoma na kuandika lakini wanafahamu mambo mengine makubwa, hivyo iwapo watafundishwa kusoma na kuandika, wanaweza kutumia utaalamu walio nao kuboresha maisha yao.

Naye Ofisa Elimu Kiongozi, kitengo cha Elimu ya Watu Wazima kutoka Wizara vya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Regina Nicholaus, alisema utekelezaji wa mpango huo utaanza Oktoba, mwaka huu, watakapokuwa wamemaliza kuandaa kitabu cha mwalimu na mwanafunzi.

Ofisa Elimu ya Watu Wazima wa Manispaa ya Dodoma, Gosbert Damazo, alisema kuwa katika Manispaa ya Dodoma, watu wanaojua kusoma na kuandika ni 137,845, sawa na asilimia 74.2 ya wakazi wote wa manispaa hii na wasiojua kusoma na kuandika ni 47,984 sawa na asilimia 25.8.

Wakichangia katika mkutano huo, wadau wa elimu walisema kuwa waratibu wa elimu wawezeshwe kupata takwimu sahihi na maana nzima ya elimu ya watu wazima.

Author:Fatma Gaffus, Dodoma
Tanzania Daima.

Tuesday, June 10, 2008

We can Buld our Own Museum



The Sitti Binti Saad Center at Mpwapwa Teachers College very near to Mpwapwa Distric court where Shaaban Bin Robert(The Author of the very famous book tittled Wasifu wa Sitti bint Saad) used to work.

Tuesday, April 29, 2008

Sunday, March 30, 2008

Upimaji huu katika Elimu hauna tija

Sasa naanza kuiamini ndoto yangu niliyowahi kuota zamani kidogo.Ndoto hiyo ilihusu kuondolewa/kufutwa kwa mtihani wa darasa la nne, kidato cha pili na kubali aina ya upimaji wa wanafunzi katika elimu ya juu hapa nchini.

Imani yangu kuwa ndoto yangu inaweza kutimia inatokana na kauli ya Amiri jeshi mkuu ambaye pia ndiye Rais wa Jamhuri yetu aliyoitoa katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa Elimu wa mwaka huu uliofanyika Ubungo Plaza mwanzoni mwa mwezi huu.Katika ufunguzi wa mkutano huo,Rais alitoa changamoto kwa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kuitaka kuangalia upya utaratibu wa mtihani wa darasa la nne na umaana wake.

Nisingependa kujiumiza kichwa kutafakari msingi wa kauli hiyo ya JK ikiwa ni ya kisiasa au kitaalam kwani kihalisia swala hilo halihitaji mtu kuwa na PhD ya Ualimu kulibaini.

Mantiki ya kuwepo au kutokuwepo kwa mtihani wa darasa la nne na ule wa kidato cha pili ni swala ambalo nimekuwa nikilizungumzia mara nyingi sana na watu ninaokutana nao na kufanya nao kazi hasa katika warsha na semina ninazohudhuria kwa muda mrefu.

Pamoja naukweli kuwa nimefarijika sana kuona kuwa mamlaka imetambua upungufu uliopo katika utekelezaji wa mfumo wetu wa elimu,nasikitika kuona kuwa walimu na waelimuisha walimu tulikuwa kimya hadi wanasiasa wanapotuaibisha majukwaani kwa kutukumbusha wajibu wetu wa “Kufikiri kwa kina kuhusu mustakabali wa Elimu na maendeleo yake hapa nchini”.

Upimaji kwa kutumia mitihani ya taifa kwa darasa la nne na kidato cha pili hauna tija kwa kuwa mitihani hiyo hupelekea hukumu ya kielimu kwa wanafunzi ambao kasi na wepesi wao katika kujifunza ni mdogo,bila kuzingatia mambo yote yanayomzunguka katika kuipata Elimu hiyo.Jambo lililopelekea/sababisha elimu yetu kuwa ya kukariri/kujiandaa kushinda mitihani na kuliacha kundi kubwa la vijana wetu wanaweza kutoa mchango mkubwa kwa taifa likipotea.Bonyeza hapa usome zaidi kuhusu swala hili

Ninapotafakari ni kwa kiasi gani taifa limeingia hasara kwa kuwapoteza vijana ambao wangeweza kutoa mchango kwa taifa letu baada ya kuchujwa na mitihani hiyo namkumbuka rafiki yangu mmoja ambaye nilipata kusoma nae shule ya msingiHuyu sio mwingine bali ni Tanzania one! {Waliohitimu meta sekondari au Mzumbe kati ya 1999-2002 wanaweza kumkumbuka}.Jamaa huyu tangu tulipoanza darasa la kwanza hakuwahi kuwemo hata katika wanafunzi 50 bora.Kwa bahati wakati huo mtihani wa darasa la nne ulikuwa umefutwa hivyo alitubeba hadi darasa la saba.

Kwa kuwa hakuchaguliwa kujiunga na shule za sekondari za serikalikama wengi tulivyokuwa tumetarajia,alilazimika kutafuta shule ya Private.Alichukua fomu na kufanya usaili katika shule za Airwing,JKT Yombo Tech,Kiabasila na Makongo.Huko kote hakupata nafasi.Baada ya kuona muda unakwisha,baba yake ambaye kwa wakati huo alikuwa akiishi na kufanya kazi Mbeya aliamua kumuita ili akafanya masomo ya ufundi huko.Haijulikani nini kilitokea.Lakini tunachofahamu muda wa usaili Meta ulikuwa umeshapita nae hakufanya usaili hapo ila shule ilipofunguliwa alivaa sare na kuingia darasani.Miaka miwili na nusu ya kwanza yote hakuonyesha mwelekeo lakini alibadilika ghafla mhula wa pili wa kidato cha tatu na mwisho wa siku mtihani wa taifa wa kidato cha nne alipata daraja la kwanza pointi 09 na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano & sita shule ya sekondari Mzumbe.Alipewa jina la Tanzania one baada ya kuwa anaongoza karibu katika kila mtihani.Na katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita alidhihirisha hilo kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza aliyefaulu vizuri zaidi kitaifa.

Huyu niliyemzungumzia hapa ni mmoja tu kati ya maelfu ya wanafunzi wenye uelewa wa pole pole ambao ukuaji wao kiakili ni wa taratibu sana ambao tumewapoteza kwa kuwa tu eti wamefeli mtihani wa darasa la nne au kidato cha pili.

Tanzania one alihitaji miaka 11 kuubainishia ulimwengu kuwa kuwa yeye nii exceptional kiakili {Gifted!?}.Ikiwa angepita katika zama hizi za mitihani ya std 4 na kidato cha 2 hakika jamaa angeishia kulima kokoa na kuuza maparachichi Mwanjelwa kama sio peremende mtaani.

Tunawahukumu wanafunzi wetu kila wanapofika darasa la nne na kidato cha pili kwa kuendelea na darasa linalofuata,kukariri/rudia darasa au kutoendelea kabisa na elimu[{Ugaidi!?}] kinyume kabisa na matarajio ya mfumo wetu wa elimu [2:7:4;2:3+] ambao unataka mtu asome na kufanyiwa upimaji tamati anapofikia mwisho wa kozi ,yaani std 7 au form 4.

Wanazuoni na wadau wote wa Elimu,Dhambi ya kutengeneza vibaka na wazururaji {kuwahukumu kwa kuwanyima fulsa ya kuendelea na masomo} tofauti na malengo ya elimu nchini tumeifanya kwa muda mrefu sasa.Ikiwa tunaikubali na kuiungama dhambi hii,ni vema sasa tukaamua kwa dhati kutoendelea kuitenda kwa kufanya maboresho yanayotakiwa.

Walimu, waelimisha walimu na wadau wote wa elimu kwa ujumla tunapaswa kuliona hili.Kwa mtazamo wangu swala la kuondolewa kwa mitihani hiyo halihitaji mjadala wala utafiti kwani dhamira/kusudio la la mfumo wetu wa elimu ni kumfanya kila anayeanza shule ya msingi au sekondari amalize sio kuishia njiani.

Labda kwa kumalizia napenda kuwakumbusha wenzangu kuwa Mheshimiwa J.K ameliona swala la mtihani wa std 4 na kidato cha 2.Sisi kama Educational Practitioners tunapaswa kwenda mbele zaidi katika kufikiri kwetu na kuangalia mfano ikiwa upimaji tamati unampima mwanafunzi katika nyanja zote tatu?( yaani nyanja ya maarifa/ufahamu,Uelekeo na Stadi) Katika hili kwangu naona kunatatizo kubwa ambalo linahitaji mjadala mpana na wa kina.Hata hivyo si vibaya nikidokeza kuwa hatuna budi kuiga kutoka kwa wengine mfano Afrika ya kusini ambao wanampatia credit mwanafunzi kadri anavyopanda darasa na inapotokea akafeli kabla ya kumaliza kozi wanamtambua(Certify) kwa kuonyesha kiwango cha darasa alichofikia .Tofauti na sisis ambapo mtu anayefanya kozi ya miaka mitano(5) chuo kikuu akishikwa 4th year hakuna anayemtambua kuwa aliwahi kufika chuo kikuu.Poleni watu mnaofanya MD.

Wednesday, March 5, 2008

Kilio cha Walimu:Ngoma isiyo na wachezaji?

Nini kikubwa mno unachoweza kututendea leo ambacho

bado hatujajitenda wenyewe?

Utatuambia nini leo ambacho bado

hatujajidanganya nacho?


Huwezi kujua ni miaka mingapi

tumezililia hadi tukaziangulia kicheko

njozi zetu zilizosambaratika na kubaki

vipande vipande.


Ndiyo

Tumeazimia kuyalazimisha matumaini

yetu yaliyokwisha potea kuwa njozi

thabiti kuliko unavyoweza kufikiri:

itangaze ukombozo wetu uliopatikana kwa

uchungu:

Kwa hiyo wala usituulize tunajishughulisha

na nini safari hii:

Mwenye ndoto haisahau hata

ijapokatishwa.

Nawe hutasalimika na hicho

tutakachokifanya.

Kutokana na vipande vya maisha yetu.



Nimeanza mada hii kwa utenzi huo wa mwanazuoni,malenga na mwanaharakati Prof.Abena Busia kwa makusudi ili kujikumbusha na kuikumbusha jamii kuhusu harakati za walimu kutafuta na kudai haki wanazostahili kutoka kwa waajiri wao(Katibu mkuu wizara ya Elimu na Wakurugenzi wa wilaya)


Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana harakati zinazofanywa na CWT kwa muda mrefu.Hii ni kutokana na ukweli kuwa siku zote huwa najitahidi sana kujustfy wazo langu nililowahi kulitoa hapo awali kuwa CWT sio chama cha kitaaluma(Rejea makala yangu kuhusu CWT na mustakabali wa Elimu nchini)


Ninaporejelea harakati za CWT hasa za viongozi wa ngazi za juu katika chama hicho,nafarijika kutambua kuwa walimu sasa wameutambua unyonge wao na sasa wanaazimia kuukana kama katiba ya chama hicho inavyoleleza katika sehemu ya utangulizi:

“KWA KUWA mwalimu ni kama raia mwingine yeyote nchini

ana haki ya kupata huduma bora za kijamii,kiuchumi

na kimaslahi kama vile afya,chakula,malazi,usafiri na

Huduma nyingine za kijamii.


Kwa hiyo BASI:Sisi walimu wote kwa pamoja tunaazimia

kuungana na kuunda chama chetu kitakachohakikisha kuwa

walimu wote tunatekeleza wajibu wetu na kupata

haki zote tunazostahili kutoka kwa waajiri wetu”


Nimeshawishika kuandika makala hii kutokana na matokeo ya kikao cha pamoja kati ya mawaziri wa TAMISEMI,Elimu,Menejimenti ya Utumishi wa umma na viongozi wa chama cha walimu kilichofanyika Febr. 22 mwaka huu chini ya waziri mkuu ambapo ilikubalika kuwa serikali itawalipa walimu madeni yao yote ifikapo mwezi huu.


Walimu,kwa hakika tuna kila sababu ya kuishinikiza serikali kupandisha mishahara yetu na kutulipa madai yetu mengine kama vile posho za kujikimu,malimbikizo ya mishahara na likizo.Hatuna sababu ya kuchuuzwa na matamshi yasiyomaanisha utatuzi wa matatizo yanayotusonga katika utekelezaji wa wajibu wetu-ndio maana Prof.Abena anatukumbusha kuwa”Utatuambia nini leo ambalo bado hatujajidanganya nacho? Je, ni miaka mingapi tumezililia shatili zetu hadi tukaziangulia kicheko?Ni matumaini yangu kuwa CWT na walimu wote kwa ujumla tumeazimia kwa dhati kuyalazimisha matumaini yetu yaliyokwisha potea kuwa njozi thabiti kuliko mtu yeyote anavyoweza kufikiri.Serikali inapaswa kutambua kuwa mwenye ndoto haisahau hata ijapokatishwa,nayo haitasalimika na kile tutachokifanya.


CWT na walimu kwa ujumla tunachangamoto kubwa katika kuhakikisha tunapata stahili zetu kutoka kwa waajiri wetu.Changamoto ya kwanza ni katika hulka ya itikadi na ya pili iko katika mikanganyiko yetu ya kiuharakati katika jumuia yetu bila kutambua kwa kina kile kinachocho tuunganisha na mipaka yake.

Kujielewa kwa namna ya kutuwezesha kubainisha na kutetete msimamo wetu ni changamoto nyingine tuliyonayo.Tunao wajibu wa kuwa wanafunzi wakati wote tukichambua bila kukoma hali ya walimu na jamii yetu katika enzi hizi za utandawazi ili kujifahamisha njia zinazotumika katika kutunyima stahili zetu na jinsi zinavyobadilika badilika.


Labda kwa kumalizi tu,niwakumbushe walimu kuwa silaha ya mwisho ya kila mfanyakazi Duniani ni kugoma pale anapoona hapati haki zake.Hatua hii ya wafanyakazi hufikiwa baada ya mwajiri kukaidi kusikiliza kilio chao kwa muda mrefu.


Alamsiki!