Thursday, November 26, 2009

Introducing "Ufundishaji wa SAYANSI: Mafunzo ya Ualimu-cheti."



Ufundishaji wa Sayansi: Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti ni kitabu kilichoandikwa kwa ustadi mkubwa na kuhaririwa kwa umahiri ili kimsaidie Mwalimu tarajali kujifunza bila shida somo la Sayansi kwa vyuo vya Ualimu hapa nchini.


Kitabu hiki ni cha kwanza katika mfululizo wa vitabu viwili vilivyoandikwa mahususi kwa ajili ya kutumika katika utekelezaji wa muhtasari wa mafunzo ya Ualimu wa Elimu ya msingi ngazi ya cheti uliotolewa mwaka 2009 na wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Katika kurahisisha ufundishaji na ujifunzaji wa somo,kitabu hiki kimejikita katika mjadala mpevu na wa kina kwa mada zote za maudhui ya ufundishaji kama zilivyoainishwa katika muhtasari huo mpya.Katika kila mada za kitabu hiki kuna vitendo vya kutosha na mazoezi yatakayomwezesha mtumiaji wa kitabu hiki kujitathimini maendeleo yake katika kujifunza.

Aidha kitabu hiki kinaweza kutumika pia mahali popote ambapo mafunzo kazini kwa walimu yanatolewa na kwa walimu walio kazini kwa lengo la kupanua uelewa wao kuhusu ufundishaji.
 ____________________________________________
 Maelezo kuhusu kitabu hiki ni kama ifuatavyo:
JINA : Ufundishaji wa
Ufundishaji wa Sayansi:Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti.

©John J. Malata, 2009

Toleo la kwanza,2009

Chapa ya kwanza Novemba,2009

ISBN 978 9987 9313 5 4

Ili kujipatia nakala yako wasiliana nami kwa anuani inayoonekana hapo chini:

Anuani:
John J. Malata
Chuo cha Ualimu Vikindu
S.L.P 16268
DAR ES SALAAM
SIMU:+255 754 351 868-Hotline
            +255 782366090
+255 653077830
+255 755 396511:-Uliza Mwl: Fuime
+255 784 988604


ZINGATIA: Atakaye nunua kitabu hiki kabla ya february 2010 atapata punguzo la asilimia ishirini la gharama halisi ya kitabu. [20% less]