Saturday, September 26, 2009

Kuinuka na Kuanguka kwa UDSM!

Kwa aliyewahi kusoma, kukipenda, kufundisha na kufanya kazi maeneo ya chuo, na yote kabisa Mtanzania mzalendo!

Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam, palikuwa mahala pa cheche ya fikra na mbubujiko wa mijadala makini na ya huru kwa maslahi ya Taifa na Afrika kwa ujumla.

Palikuwa mahala pa ndoto ya kila kijana kuweza kufika na kupata fursa ya kusoma hapo. Ilikuwa ndoto na fahari ya kila mzazi kuweza kumfikisha mtoto wake hadi ngazi hiyo. Ilikuwa ndoto kwa wanataaluma (wa ndani na nje ya Tanzania) kupata fursa kufundisha katika chuo hicho. Mlimani palikuwa kizio cha kupima taaluma ya juu nchini!

Hakika waswahili walisema “hakuna marefu yasiyo na ncha”! na kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho! Kama kilivyoanza kwa juhudi za dhati ndivyo kinavyomalizwa kwa juhudi za dhati na kundi la watu wachache wasiotaka kusikia la mwazini wala mnadi swala wakiwa na kiburi cha nguvu ya vyombo vya dola na ushosti wa wakuu wa nchi.Soma makala Hii ya kupendeza kwa kubonyeza HAPA. Kama ilivyoandikwa na Asha Miguubaja na kupostiwa na Chambi Chachage katika bogu ya  

UDADISI: Rethinking in Action

No comments: