Wiki iliyopita wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi ilitoa miongozo mipya [Sylabus] kwa ajili ya kufundishia katika vyuo vya Ualimu kwa ngazi zote za cheti na stashahada. Pamoja na ukweli kuwa kwa kiasi fulani upimaji katika somo la Sayansi kwa njia yaVitendo umezingatiwa katika muhtasari hiyo Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni umebainisha kuwa vyuo vya Ualimu 16 vya serikali hapa nchini havina maabara kwa ajili ya mafunzo ya somo la sayansi kwa vitendo.Kutokana na hali hiyo kwa muda mrefu sasa Balaza la Mitihani la Taifa limekuwa likiwatahini walimu katika ngazi ya Diploma na Cheti kwa njia ya Nadharia jambo linalopelekea kufa kwa misingi ya Sayansi kwa wanafunzi na walimu wetu.
Kama wadau wa Elimu hapa nchini tufanye nini kurekebisha hali hii? TAFAKARI!!!!
WAZIRI KIKWETE: MFUMO MPYA KUWEZESHA WATANZANIA KUPATA FURSA ZA AJIRA NJE
YA NCHI
-
Na Mwandishi Wetu; Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye
Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesema katika mwaka wa...
11 hours ago
No comments:
Post a Comment